Breaking

PAKUA MCHAINA APP HAPA CHINI USOME HABARI ZETU HATA USIPOKUWA NA MB

Friday, September 1, 2017

JOB VACANCIES AT ULANGA DISTRICT MOROGORO






TANGAZO LA KAZI ZA WADADISI KATIKA MKOA WA MOROGORO.

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inawatangazia watanzania wenye sifa zilizoainishwa hapo chini kuleta maombi yao ya kazi ya muda ya udadisi au ukusanyaji wa takwimu kwa ajili ya Utafiti wa Kilimo wa Mwaka 2016/17. Utafiti huu unahitaji mwombaji atoke kwenye mkoa ambao utafiti unafanyika.

Waombaji wanatakiwa kuwa ni watanzania wenye sifa zifuatazo;

a)      sifa za msingi:-
                               i.             Umri wa miaka 18 na kuendelea,
                             ii.             Elimu ya kuanzia  Kidato cha Nne,
                          iii.            Mkazi kutoka katika Mkoa husika.

b)     sifa za ziada:-

                               i.             Elimu ya Cheti cha Ukusanyaji Takwimu rasmi kutoka Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika (EASTC),
                             ii.            Uzoefu wa kazi ya kukusanya takwimu katika tafiti mbali mbali zilizofanywa na NBS,
                          iii.            Uzoefu wa kufanya Utafiti wa Kilimo wa Mwaka 2014/15.

Barua za maombi ziandikwe kwa mkono wa mwombaji akionesha anuani kamili na namba yake ya simu pamoja na kuambatisha nakala ya vyeti vyote vya elimu na mafunzo, wasifu wa mwombaji (CV).
                                              
Maombi yatumwe kabla ya  tarehe 09/09/2017 kwa kupitia anuani ifuatayo:

Meneja Takwimu wa Mkoa,
Ofisi ya Taifa ya Takwimu,
S. L. P. 581
MOROGORO.
                                                                      
      NB:  i. Tangazo hili linapatikana kupitia www.nbs.go.tz pamoja na www.eastc.ac.tz

               ii. Wale watakaochaguliwa kwa ajili ya usaili ndio watakaoitwa. NBS haitahusika na   gharama za kuja kwenye usaili huu.


                                                                       IMETOLEWA NA
MKURUGENZI MKUU
OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU
24 August, 2017