TAARIFA
KWA UMMA
WANAFUNZI
WA MWAKA WA KWANZA WALIOTHIBITISHWA
KUHAMA
PROGRAM AU VYUO
Tume
ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inautangazia Umma kuwa zoezi la kupokea na
kuthibitisha maombi ya uhamisho wa wanafunzi wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa
masomo 2016/17 limekamilika. Orodha ya wanafunzi waliothibitishwa na TCU
imeshawasilishwa kwenye vyuo husika. Hivyo, wanafunzi wote waliotuma maombi ya
uhamisho wanaweza kuona matokeo ya uhamisho wao kupitia linki ifuatayo: (BOFYA HAPA KWA INTER UNIVERSITY na BOFYA HAPA KWA INTERNAL UNIVERSITY)
Hata hivyo, Tume
inapenda kuwatangazia wanafunzi wote waliotuma maombi ya uhamisho kwamba:
•
Wanafunzi wote waliothibitishwa kuhama
vyuo wanatakiwa wawe wamesharipoti kwenye vyuo husika kwa usajili na taratibu
nyingine kabla ya muda wa usajili kwisha;
•
Wale ambao hawataona majina yao katika
orodha ya uhamisho watambue kuwa uhamisho wao haujathibishwa na Tume hivyo
wanashauriwa kubaki kwenye vyuo walivyochaguliwa awali;
•
Wanafunzi waliohama bila kuidhinishwa
hawatatambuliwa na Tume;
•
Muda wa kupokea na kuthibitisha maombi
ya uhamisho ulikwisha tarehe 18 Desemba, 2016. Hivyo, Tume haipokei tena maombi
ya uhamisho toka Taasisi yoyote ya Elimu ya Juu.
•
Majina ya wanafunzi wote waliohama
yamewasilishwa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kwa ajili ya kumbukumbu zake.
Imetolewa
na
Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania 3/1/2017
No comments:
Post a Comment